Wadau wa michezo wammwagia sifa Rais Samia katika mwaka moja

 Na. John Mapepele

Watoa mada mbalimbali kwenye kongamano la kuelezea mafanikio ya michezo wametoa shuhuda na kupongeza mageuzi na mapinduzi makubwa huku wakisema  mama Samia ameupiga mwingi na kuondoka nao.

Aliyeanza ni Katibu Mkuu. Dkt, Hassan Abbasi ambaye amesema Mhe. Rais amekuwa na utashi wa kisiasa kwenye michezo, amefanya uwekezaji mkubwa na kuboresha na kujenga  miundombinu za michezo.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa watu wenye Ulemavu (TAFF) Peter Sarungi amefafanua kuwa kutokana na maono makubwa ya Mhe. Rais timu yao imefuzu kwenda kombe la dunia.

Aidha, ameongeza kuwa kutokana na utashi huo Mhe. Rais amefungua ajira kubwa za kitaifa na kimataifa kwa wachezaji walemavu.

Amesema hadi sasa wachezaji wanne (4) wameshapata timu katika mataifa mbalimbali duniani.

Kaimu Katibu Mkuu  wa Shirikisho la Riadha  Jackson  Ndaweka amesema mashindano ya taifa ya riadha  yameweza kufanyika kwa mafanikio makubwa.

"Tunashukuru sana mama sasa tumeanza kupata udhamini kwa mashindano yetu kutoka katika  mashirika ya Serikali"








Post a Comment

Previous Post Next Post