
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Bi. Tone Tinnes mara baada ya kufanya mazungumzo jijini Dar es Salaam Juni mosi, 2026.
………
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Bi. Tone Tinnes. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam Juni mosi, 2026.
Katika mazungumzo hayo, Dkt. Muyungi ameishukuru Serikali ya Norway kwa ushirikiano wa muda mrefu waliouonesha kwa Serikali ya Tanzania katika sekta mbalimbali na kwa nyakati zote.
Alisema kuwa Serikali chini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua mchango wa nchi hiyo katika usimamizi mwa mazingira na kuhimili mabadiliko ya tabianchi.
Dkt. Muyungi alitaja moja ya alama ya mchango wa Norway ni kuanzishwa kwa Kituo cha Study za Mabadiliko ya Tabianchi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kunzishwa kwa Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais.
Kwa upande wake Balozi Mhe. Tonnes alisema kuwa Norway itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais katika masua mbalimbali yahusuyo sekta ya hifadhi ya mazingira.
Miongoni mwa maeneo ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili ni pamoja na Programu ya kuijengea uwezo NCMC ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuwafikia wadau wengi zaidi.
Balozi Tinnes alisema pia Serikali ya nchi yake iko tayari kuwezesha utekelezaji wa ajenda ya Mheshimiwa Rais ya Nishati Safi ya Kupikia ili kufikia lengo asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi yabkupikia ifikapo mwaka 2034.
Halikadhalika, katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kutokana na uzalishaji wa gesijoto, Norway itaendeleza ushirikiana na Tanzania katika teknolojia na matumizi ya magari ya umeme