Burundi watua Dar kushiriki tamasha la kitaifa la Utamaduni.

Na John Mapepele

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Maji na Madini nchini Burundi  ndugu Selemani  Khamissi ambaye pia ni mmiliki wa  kikundi maarufu cha taarabu nchini  humo cha Alwatan  kinachoshiriki kwenye Tamasha la Kitaifa  la Utamaduni ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuandaa   tamasha hilo huku akisisitiza kuwa tamasha hilo litaitangaza  vema Tanzania duniani.

Akiongea na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na michezo. Saidi Yakubu ofisini kwake jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili amesema Serikali ya Burundi inaunga mkono jitihada za serikali ya Tanzania katika  kuenzi na kuendeleza  utamaduni ndiyo maana  wasanii kutoka Burundi wanashiriki  katika tamasha hili.

“Naomba nisema nimefurahi kuja Tanzania kushiriki kwenye tamasha tunawahidi watanzania wajitokeze kwa wingi kwa ajili ya kuja kuona uzoefu wetu kwenye taarabu kwa kuwa Burundi ina hazina kubwa ya magwiji wa taarabu kutoka miaka mingi.”amesisitiza  Khamissi

Akiwa ofisini hapo Khamissi amepata fursa ya kutembelea Uwanja wa Benjamin Mkapa  pia kuangalia maandalizi yanayoendelea ambapo ameelezea kuwa uwanja huo una hadhi ya kimataifa.

Akimtembeza kwenye miundombinu ya uwanja hui  Yakubu amesema maandalizi kwa ajili ya tamasha hilo yamekamilika


 

Post a Comment

Previous Post Next Post