Waziri Dkt.Damas Ndumbaro Akutana Na Wadau Wakubwa Wa Utalii Nchini Uhispania

 

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), akiwasilisha mada kuhusu utalii wa Tanzania wakati wa mkutano wake na wadau wakubwa wa utalii wa nchini Uhispania Machi 8, mwaka 2022 katika ukumbi wa Exe hotels nchini Uhispania
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Damas Ndumbaro (aliyevaa shati linalotangaza utalii) akiwa na Balozi Samwel W. Shelukindo ambaye ni  Balozi wa Tanzania na Uhispania, wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wakubwa wa utalii wa Uhispania.


Dkt. Damas Ndumbaro ambaye niWaziri wa Maliasili na Utalii leo Machi  8, 2022 amekutana na wadau wakubwa wa Utalii kutoka nchini Uhispania na kufanya nao mkutano kuhusu fursa mbalimbali za utalii na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania.

Mkutano huo umeandaliwa na Ubalozi wa Tanzania - Paris unaowakilisha pia Uhispania pamoja na Shirika la Utalii Duniani.

Wadau hao, walionyesha ari kubwa ya kuendelea kushirikiana na Ubalozi ili kupeleka idadi zaidi ya watalii kutoka Uhispania.

Post a Comment

Previous Post Next Post