Leo tarehe 15/6/2022 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewafikisha watuhumiwa wawili Raia wa China Bw. Zhu Wei na Bw. Tao Pan katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kwa makosa ya kukutwa na bidhaa ambazo hazijafuata taratibu za forodha, kukwepa kodi na uhujumu uchumi. Mashtaka hayo yamesomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Mhe. Rita Tarimo ambaye ameiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 29/6/2022.
TRA YAWAFIKISHA MAHAKAMANI WACHINA WAWILI, ZHU WEI NA TAO PAN
byJMABULA BLOG
-
0