BRELA YAENDELEA KUTOA ELIMU KATIKA MAONESHO YA BIASHARA YA NCHI ZILIZO JILANI NA ZIWA TANGANYIKA MKOANI KIGOMA

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Bi. Latifa Khamis (kushoto) na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bi. Stella Kahwa (kulia) wakipata maelezo kutoka kwa Afisa Usajili wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Angela Kimario kwenye maonesho ya Biashara ya chi zilizo jirani na ziwa Tanganyika yanayokwenda sambamba na Kongamano la Biashara. Maonesho na kongamano hilo linafanyika mkoani Kigoma kwa kushirikisha nchi za Burundi, Rwanda, Congo, zambia na mwenyeji Tanzania ambapo yatahitimishwa Mei 13, 2022.


 Afisa Usajili kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni(BRELA) Bi. Angela Kimario akiwahudumia wadau waliofika katika dawati la BRELA kwenye maonesho ya biashara ya nchi zilizo jirani na ziwa Tanganyika yanayokwenda sambamba na kongamano la Biashara mkoani Kigoma. Maonesho hayo yanayohitimishwa Mei 13 2022, yameshirikisha nchi za Rwanda, Burundi, Congo, Zambia na mwenyeji Tanzania.

Post a Comment

Previous Post Next Post