Maafisa Utamaduni na Michezo tekelezeni maagizo ya Waziri Mkuu kwa Vitendo - Mhe Mchengerwa


Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni,  Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amewataka Maafisa Utamaduni na Michezo  kutekeleza maelekezo yote aliyoyatoa Waziri Mkuu jana Aprili 5, 2022 wakati akifungua  kikao kazi cha maafisa hao na  kuwataka  kutumia utaalaam  wao kufanya kazi kwa weledi Katika kuendelea kuwapa  furaha  watanzania.

Mhe. Mchengerwa amesema hayo leo Aprili 6, 2022 wakati alipokuwa akimkaribisha Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Innocent Bashungwa kufunga kikao hicho cha siku tatu kilichojadili mambo mbalimbali ya sekta hizo.

“Naomba nendeni mkawe karibu na wananchi pia muwe wanyeyekevu kwa sababu tukiwa karibu na wananchi mambo  mengi yatakwenda  vizuri” amesisitiza Mhe. Mchengerwa.



Akizungumzia  kuhusu uwajibikaji amesema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alihusia   kila mtu akitekeleza wajibu wake maendeleo ya haraka yanawezekana ambapo ametoa wito,  kwa maafisa hao kwenda tufanya mageuzi  ya tasnia hizo  kwa weledi.

Mhe. Mchengerwa ametumia muda huo kumhakikishia Mhe. Waziri Mkuu Majaliwa  kutekeleza  maelekezo yote kwa kushirikiana na wadau wote ikiwa ni pamoja na TAMISEMI.

Amesema kuanzia sasa  kila afisa  atapimwa  kutokana na utendaji wake katika kuratibu.

Pia amesema   karibuni  atazindua program ya mawasiliano ambayo wadau mbalimbali wa sekta wataweza kuwasiliana  moja kwa moja na yeye ili kujadiliana na kupata ufumbuzi wa changamoto.


Naye Naibu Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Saidi Yakubu amesema  kikao hicho kimekuwa na mafanikio makubwa  ambapo mada mbalimbali zilijadiliwa.

Amezitaja mada  zilijadiliwa kuwa ni pamoja na mwongozo  wa uendeshaji wa matamasha ya utamaduni, uratibu na usimamizi wa matamasha  ya Utamaduni katika Halmashauri za Wilaya na Mikoa.

Mada nyingine ni uibuaji na uendelezaji wa vipaji na kuongeza fursa za ajira kupitia sekta za u

Utamaduni, Sanaa na Michezo katika ngazi ya mtaa kwa mtaa.

"Lazima tujipange ili tupeleke timu nyingi katika mashindano ya kimataifa. Twendeni tukafanye mapinduzi kwa pamoja"Amesisitiza Naibu Katibu Mkuu, Yakubu.


Post a Comment

Previous Post Next Post