Kinana aipongeza Wizara kwa kuhifadhi Utamaduni wa Ukombozi wa Bara la Afrika


Na John Mapepele

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara. Mhe, Abdulrahman Kinana leo Aprili 20, 2022 ametembelea Ofisi za Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika jijini Dar es Salaam na kupongeza juhudi kubwa zinazofanywa na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo baada ya kupata maelezo ya Waziri anayeisimamia Wizara hiyo, Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Mhe. Kinana amesema Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ndiyo uti wa mgongo wa taifa lolote na kusifu jitihada zinazofanywa na Wizara kwenye kuhakikisha  utamaduni wa kiukombozi wa Bara la Afrika  unaenziwa na kuhifadhiwa kwa faida ya sasa na  vizazi vijavyo.

Kwa upande wake, Waziri Mchengerwa amefafanua kuwa mpango wa Serikali kwa sasa  ni kujenga makumbusho kubwa ya kisasa.


Aidha, amesema  programu  inaendelea  na kushirikiana  na Wizara ya Maliasili na Utalii kukamilisha mchakato wa kuyatangaza maeneo15 ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika yaliyopo nchini kuwa Urithi wa Taifa  kwa kuyatangaza  kwenye gazeti ya Serikali ili yalindwe kisheria.

Mhe. Mchengerwa amesema  Programu hii pia  inayomajukumu mengi lakini kubwa zaidi ni kuhakikisha ina enzi, kulinda, kuendeleza, kuhifadhi na kutangaza urithi wa ukombozi wa Bara la Afrika uliopo nchini na Afrika kwa ujumla.

Ameongeza kuwa kutokana na jukumu hili ambalo Tanzania imekabidhiwa hivyo ina wajibu wa kuukumbusha umma wa Afrika kuhifadhi tunu hizi muhimu ili vizazi vijavyo vitambue  waafrika ni ndugu na wanaoishi katika misingi hiyo tangu kipindi cha ukoloni hadi kupatikana kwa uhuru wao.


 

Post a Comment

Previous Post Next Post