HAFLA YA UVISHWAJI VYEO KWA VIONGOZI WA NCAA NA TANAPA

 


Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro leo tarehe 18 februari, 2022 ameongoza zoezi la uvishaji vyeo kwa Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa  Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA).

Viongozi waliovishwa vyeo hivyo ni William Mwakilema ambaye hivi karibuni aliteiliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Hifadhi za Taifa (TANAPA).

Viongozi wengine waliovishwa vyeo ni kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) ambao ni Bw. Needpeace Wambuya aliyepandishwa cheo kuwa Naibu kamishna wa Uhifadhi (Huduma za Shirika) na Bw. Elibariki Bajuta aliyepandishwa cheo kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi (Huduma za Ulinzi)

Post a Comment

Previous Post Next Post