Na John Mapepele
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Mohamed Mchengerwa na Katibu Mkuu wake Dkt. Hassan Abbasi wameshiriki kwenye hafla ya usiku wa Mahaba ndi ndi ndi leo Februari 14, 2022 jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo imeratibiwa na WASAFI kwenye siku ya wapendanao duniani kudumisha upendo na amani miongoni mwa familia.
Wasanii wakongwe wa muziki wa kizazi kipya wametumbuiza katika hafla hiyo na kuifanya hafla hiyo kuwa na radha ya aina yake.