WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUSHIRIKIANA NA TAMISEMI KUKABILIANA NA WANYAMAPORI WAKALI NA WAHARIBIFU

 

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akijibu swali la Mbunge wa Meatu, Mhe.Leah Jeremiah Komanya ambapo amesema Serikali itaendelea kutenga fedha za ununuzi wa vitendea kazi ikiwemo magari ili kukabiriana na changamoto za wanyamapori wakali na waharibifu.
………………………………………………………………..
Naibu waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja amesema Wizara itashirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI kujenga uwezo wa Halmashauri kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu.
Mhe. Mary Masanja ameyasema hayo leo Bungeni jijini Dodoma wakati wa akijibu maswali ya wabunge kuhusu hatua na mikakati mbalimbali inayoendelea kuchukuliwa na Wizara kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu akibainisha kuwa  Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA)  imeongeza watumishi 87 sawa na ongezeko la asilimia 40 ili kuimarisha usimamizi wa maeneo ya mapori ya akiba katika  wilaya za Meatu na Itilima.
Aidha, amesema Wizara itaendelea kuimarisha na kuendeleza tafiti na kutumia mbinu mbalimbali za  udhibiti  na ufuatiliaji wa makundi ya tembo ikiwemo kuwafunga mikanda maalum ya kielektroniki  ya kufuatilia mienendo ya makundi korofi ya tembo,   kufundisha  na kuviwezesha vikundi vya  wananchi kufuatilia maeneo walipo tembo, matumizi ya ndege zisizokuwa na rubani, kutengeneza minara  ya kuangalia mbali, matumizi ya mizinga ya nyuki na vifaa vyenye mwanga mkali pamoja na kuwahamasisha wananchi  kutoa taarifa mapema  pindi wanapovamiwa na wanyamapori hao

Post a Comment

Previous Post Next Post