TAWA YASHIRIKI KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MJINI MOROGORO

 


………………………………………………………………………………..

. NA FARIDA SAID MOROGORO

Maafisa na Askari wa Uhifadhi wa TAWA wameshiriki katika maandamano ya kusherehekea siku ya wanawake Duniani
Watumishi hao waliongozwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi Bi.Gloria Bideberi
Akizungumza katika siku hiyo ya wanawake Mkuu wa wilaya ya Morogoro Bw.Bakari Msulwa amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa fursa na kuwaamini zaidi wanawake na watoto wa kike katika nafasi za uongozi, siasa, masomo na katika taasisi za umma kwa kuwa siku zote wameonesha upendo, uchapakazi, uzalendo, umakini na utekelezaji uliotukuka.
Aidha amesema Serikali imetekeleza kwa kivitendo na itaendelea kufanya hivyo katika ujenzi wa miradi ya mbalimbali kwani siku ya wanawake wameendelea kuvunja rekodi ya kushiriki katika kazi mbalimbali za kujenga Taifa.

Aidha,Kwa upande wa TAWA Kamishna Msaidizi Mwandamizi Bi.Gloria Bideberi alizungumza na wandishi wa habari amesema TAWA inaadhimisha siku ya wanawake kwa kushirikiana na taasisi nyingine huku akitoa wito kwa watumishi wote wanawake kujali na kupenda kazi zao wawapo kazini.
hatimaye baada ya shughuli hiyo Bi.Groria aliwaongoza watumishi kwenda kupata vinywaji na kukata Keki ikiwa ni sehemu ya sherehe ya kujipongeza.

Post a Comment

Previous Post Next Post