Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi, akiwa katika mazungumzo na Bw. Lorenzo Guadagno wa Sekretarieti ya Santiago Network pamoja na ujumbe ulioambatana nao, pembeni mwa mkutano wa SB64 mjini Bonn, Ujerumani.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mtaalamu wa Ushirikishwaji wa Wanachama wa Sekretarieti ya Santiago Network, Bw. Lorenzo Guadagno baada ya mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano na kuhakikisha Ofisi ya Kanda ya Santiago Network kwa Afrika iliyopo Dar es Salaam inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kufikia malengo yaliyowekwa.

………..,… 

Wadau wa mazingira kutoka Taasisi ya Hanns R. Neumann Stiftung (HRNS) ya Ujerumani wameonesha nia ya kuwekeza na kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo endelevu ikiwemo uhifadhi wa mazingira, nishati safi, biashara ya kaboni, maendeleo ya vijana na kilimo.

Nia hiyo imebainishwa katika mazungumzo kati ya Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa HRNS, Bw. Olaf Tschimpke, yaliyolenga kutafuta maeneo mapya ya ushirikiano kati ya taasisi hiyo na Serikali ya Tanzania.Kikao hicho kimefanyika pembezoni mwa Mkutano wa 64 wa Wataalam wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (SB64) unaofanyika Bonn, Ujerumani.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Muyungi aliwasilisha vipaumbele vya Taifa vilivyomo katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ikiwemo maendeleo ya masoko ya kaboni, nishati jadidifu, uchumi wa buluu, nishati safi ya kupikia na ushiriki wa vijana katika uhifadhi wa mazingira. Aidha, Dkt. Muyungi alieleza umuhimu wa kupata wadau wa kusaidia kuendesha Kituo cha Vijana cha Afrika cha Majadiliano ya Mabadiliko ya Tabianchi kilichopo Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Bw. Tschimpke alisema HRNS ina uzoefu wa kusaidia wakulima wadogo wa kahawa, kulinda mazingira na kuwawezesha vijana katika nchi mbalimbali za Afrika, ikiwemo Tanzania, Uganda na Ethiopia.

Maeneo yaliyotajwa kuwa na fursa za ushirikiano ni pamoja na kusaidia wakulima wadogo wa kahawa, kuanzisha Muungano wa Kudhibiti Uchafuzi wa Plastiki nchini, kuendeleza masoko ya kaboni, uwekezaji katika nishati ya jua, programu za michezo kwa vijana, mafunzo ya mazingira na ujasiriamali kwa vijana pamoja na uwekezaji katika teknolojia za usafiri wa umeme (e-mobility).

Pia, pande hizo mbili zimekubaliana kuendelea na mazungumzo kupitia kikao cha ufuatiliaji kitakachofanyika mwezi Julai mjini Bonn, Ujerumani, pamoja na kuandaa Hati ya Makubaliano (MoU) itakayobainisha maeneo ya ushirikiano na utekelezaji wake.

Vilevile, imekubaliwa kuandaliwa kwa mkutano wa wadau utakaowakutanisha washirika wa HRNS na Serikali ya Tanzania nchini Tanzania ili kujadili kwa kina fursa za ushirikiano, uwekezaji na utekelezaji wa maeneo yaliyobainishwa kuwa na maslahi ya pamoja.Katika hatua nyingine, Dkt. Muyungi, amekutana