KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YARIDHISHWA NA USAFISHWAJI WA MRADI WA BWAWA LA NYERERE (JNHPP).

 

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja (Wa kwanza kulia) akiwa pamoja na  Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii pamoja na Viongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) wakikagua maeneo  mbalimbali ya ujenzi wa Bwawa la kufua umeme la (JNHPP-MW2115)  wakati wa  ziara ya viongozi hao ya  kukagua eneo ambalo  miti yake inatakiwa kung’olewa ili kupisha ujenzi wa Bwawa la maji kwa ajili ya kufua Umeme.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja, Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya  Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na baadhi ya viongozi wa Taasisi za Uhifadhi za Wizara ya Maliasili na Utalii wakiangalia kazi inayoendelea  ya ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme  wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua Hifadhi ya Taifa ya Nyerere pamoja  kuangalia zoezi la  ung’oaji wa miti katika eneo hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi ya  Maliasi na Utalii, Dkt. Aloyce Kwezi (wapili kulia) akielezea umuhimu  wa Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha inaweka vivutio vya Utalii vitakavyo zunguka eneo la Bwawa la Kufua Umeme la  Julius Nyerere pindi litakapokamilika ili kuvutia wageni wengi zaidi wakati wa ziara ya kamati hiyo katika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere mkoani Morogoro. Wa pili Kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja,  Kamishna wa Uhifadhi, Prof. Dos Santos Silayo ( wa kwanza kushoto) na wajumbe wengine walioshiriki katika ziara hiyo

Post a Comment

Previous Post Next Post