WAAJIRIWA WATAKIWA KUWASILISHA TIN NAMBA KWA WAAJIRI WAO

 




Mkurugenzi wa elimu kwa mlipa kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)leo  jijini Dar es Salaam leo.

Na Ripota wetu, Michuzi TV

MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) imewataka waajiriwa wote ambao wanalipwa mshahara kwa payroll  kuwa na TIN namba na kuziwasilisha kwa waajiri wao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam leo, Mkurugenzi wa elimu kwa mlipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA,) Richard Kayombo amesema kuwa kuanzia mchakato hua umeanza mwezi Agosti, 2020 na mwisho wa kuwasilisha TIN hizo ni Desemba 31, 2020.

 "Mtumishi ambaye ameajiriwa popote pale anatakiwa kupata TIN namba na kuiwasilisha kwa mwajiri wake." Amesema Kayombo.

Hata hivyo amesema kuwa  mwajiriwa ambaye amepoteza TIN namba au hana afike ofisi za TRA ili aweze kupata TIN nyingine na kwa ambaye hana kabisa atembelee tovuti ya TRA ili aweze kuipata.
 
"Zoezi hili ni la watumishi walioajiriwa popote pale wawasilishe TIN kwa mwajiri litadumu hadi Desemba 31,2020, kwahiyo waajiri wote tumeshawaagiza wahakikishe wafanyakazi wao wamewasilisha TIN zao."

Na kwa mwajiriwa ambaye  hakuweza kupeleka TIN Kwa mwaajiri wake hataweza kupata mshahara ifikapo Januari mosi, 2021.

Kayombo amesema kuwa hakuna haja ya kuongeza muda kwa kuwasilisha TIN au kodi za mshahara kwa sababu TIN hizo zinawasikishwa kwa njia ya mtandao popote mtu alipo anaweza kuwasilisha.

"Kwa kipindi hiki tumerahisisha kwa kila mtu kutumia mtandao ili kuondoa usumbufu kwa mtu yeyote kufika ofisi za TRA." Amesema Kayombo.

Hata hivyo Kayombo amesema kuwa kampeni ya Mlango kwa Mlango imeendelea kuwafikia watu wengi zaidi.

Amesema kampeni ya Mlango kwa mlango kwa Septemba watafanyia kazi katika mikoa michache ambayo ni Arusha, Mtwara, Kagera Tabora na Mkoa wa Dar es Salaam watafanyia kazi katika wilaya ya Ubungo.

Amesema Kampeni ya Mlango kwa Mlango ni mahususi kuwafikia walipa kodi katika biashara zao na kutomsumbua mfanyabiashara kufika katika Ofisi za TRA.

Post a Comment

Previous Post Next Post