TRA YAENDESHA ZOEZI LA ELIMU KWA MLIPAKODI ARUSHA

 Mkuu wa Mkoa wa Ausha akizindua rasmi Kampeni ya Elimu kwa Mlipakodi iliyoanza rasmi tar.7sep2020 mkoa wa Arusha lengo likiwa ni kujenga ukaribu kati ya TRA na wafanyabiashara.Afisa msimamizi kodi mkuu James Ntalika kutoka kitengo cha Elimu kwa mlipakodi TRA makao makuu Dar es Salaam,na Eugeni Mkubo kutoka TRA Arusha wakitoa elimu kwa wafanyabiashara katika maeneo ya stendi ndogo mkoani hapa. Robert Tarimo mfanyabiashara wa duka na.360 ameishauri TRA mara baada ya kupatiwa elimu ya mkipakodi kwamba kabla ya kuwakadiria kodi ni vyema wakawatembelea ili waweze kuwakadiria kutokana na biashara zao Afisa msimamizi kodi mkuu James Ntalika kutoka kitengo cha Elimu kwa mlipakodi TRA makao makuu Dar es Salaam,akitoa elimu ya mlipakodi kwa mfanyabiashara Alphonce Chaki katika eneo la stendi ndogo iliyopo Jijini Arusha.Afisa TRA kutoka makao makuu Jijini Dar es salaam Juliety Kidemi akiendelea kutoa elimu ya mlipakodi kwa mfanyabiashara mwenye duka no 266 Maria Hassan Matoto.Afisa TRA kutoka makao makuu Jijini Dar es salaam Mercy Macha akiendelea kutoa elimu ya mlipakodi kwa mfanyabiashara mwenye duka no 132 maeneo ya stend ndogo Jijini Arusha .


TRA YAENDESHA ZOEZI LA ELIMU KWA MLIPAKODI ARUSHA

Na.Vero Ignatus.

Mamalaka ya mapato imeendesha kampeni ya elimu kwa mlipa kodi kwa muda wa wiki moja katika mkoa wa Ausha dhumuni kubwa likiwa ni kuhamasisha umma katika uelewa wa masuala ya kodi ili waweze kutimiza wajibu wao kisheria wa kulipa kodi 

Akizindua kampeni hiyo mkuu wa mkoa wa Arusha Idd Kimanta, amewasisitiza TRA wahakikishe kwamba ,kampeni hiyo ya elimu kwa mlipakodi inafanyika katika mkoa wote ,na wasikazanie mjini tu bali waende katika wilaya zote 6 ndani ya mkoa,sekta zote,zikiwemo za utalii ,kilimo ,ufugaji,na wafanyabiashara wa aina zote na wananchi wote wanaopaswa kulipa kodi. 

Alisema kuwa kodi ya mapato inamanufaa makubwa kwa nchi ,ambapo miradi mbalimbali imekuwa ikitekelezwa na serikali,amesema miradi mikubwa ya kimkakati na ile ya kimaendeleo, inayosimamiwa na serikali kwa maelekezo ya Rais Magufuli inatokana na kodi zinazolipwa

''Miradi hiyo ni kama bwawa la umeme la Mwl.Nyerere,Treni ya mwendokasi,ununuzi wa ndege kubwa za abiria ,ujenzi wa miundombinu ya barabara kama vile fly overs za kuunganisha mikoa na ''Kimata

Kimanta alisema ukusanyaji wa kodi unafanyika nchi nzima kupitia TRA,ambapo mkoa wa Arusha ni miongoni mwa mikoa ambayo imekuwa ikifanya vizuri katika makusanyo ya kodi, licha ya changamoto mbalimbali ,katika kipindi cha mwaka uliopita 2019/20 walikusanya jumla ya shilingi Bil.420.83 ikiwa ni ongezeko la 12% ukilinganisha na kipindi kama hiki kwa mwaka wa fedha uliopita.

Akizungumza Afisa msimamizi kodi mkuu James Ntalika kutoka kitengo cha Elimu kwa mlipakodi TRA makao makuu Dar es Salaam,anasema lengo lao ni kuweka ukaribu kati yao na wafanyabiashara ambapo zoezi hilo ni la nchi nzima.

Amesema ipo mikoa ambayo wameshaenda tayari ,kwa Arusha wameanza zoezi hilo 7sept 2020 na litafanyika katika katika wilaya zote na vitongoji vyake, na watachukua maoni kwa wafanyabiashara,kushughulikia matatizo ya wadau wao na kuwa daraja,pia amewataka kuondokana na ile dhana kwamba TRA ni inatisha au kufunga maduka na kukimbia.

Amesema mambo ambayo wanatolea elimu ya mlipakodi ni pamoja na utunzaji wa kumbukumbu,mauzo kwa siku ,manunuzi na matumizi,hiyo itamrahisishia mlipakodi kupata kodi stahiki wakati anafanyiwa makadiriao, kuliko kukisiwa kwani atajikuta analipa kiasi ambacho sicho chenyewe.

Amesema changamoto kubwa waliyokutananayo katika kuwatembelea wadau hao, ni pamoja na kutokutungika TIN namba zao katika maeneo yao ya biashara,wengine wanasema kuwa zipo nyumbani ama kwenye droo,hawatunzi kumbukumbu.

Kwa upande wake mfanyabiashara aliyepatiwa elimu ta mlipakodi na TRA Winnie Frank ameiomba Mamlaka hiyo kuwaangalia kwani kodi ni kubwa kwa sasa kulingana na kipato wanachokipata kwani biashara ni ngumu na wateja hakuna

Amesema wafanyabiashara wanakwepa na wanafunga maduka kwasababu kodi ni kubwa sana kuliko kile wanachokipata,amewaomba TRA watoze kodi kulingana na kile mfanyabiashara anachokipata itawarahisishia wao kulipa kodi.

Kwa upande wake Robert Tarimo mfanyabiashara wa duka na.360 ameishauri TRA, mara baada ya kupatiwa elimu ya mlipakodi, kwamba kabla ya kuwakadiria kodi ni vyema wakawatembelea ,ili waweze kuwakadiria kulingana na biashara wanazoziendesha.

''Sisi wafanyabiashara tunavyokwenda pale,tunapoongea na wale maofisa pale tunazungumza kulingana na biashara,mara nyingi hawatuamini kwamba biashara ipo kama unavyowaeleza,kwahiyo naomba waje watutembelee kwenye biashara zetu waangalie na yale makadirio''alisema Robert.

Post a Comment

Previous Post Next Post