TFRA YATOA MAFUNZO KWA VITENDO KWA WAKULIMA KUHUSU MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA


Zaidi ya wakulima  6o  wamefika katika vipando vya Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA)   vilivyopo katika  viwanja  vya  Nanenane Nzuguni jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza  kwa vitendo matumizi sahihi ya mbolea na mbinu bora za kilimo kwa ujumla.   Wakulima hao wamejionea tofauti   iliyopo kati mazao yaliyowekwa mbolea na yasiyowekwa  hivyo kuelezwa umuhimu wa
kuongeza tija katika uzalishaji  wa mazao kwa kuzingatia mambo muhimu ikiwemo  kutumia mbolea kwa wakati sahihi,  kwa kiwango sahihi,  chanzo sahihi na  mahali sahihi.
Bi. Schola Mbalila, 
Kaimu Meneja wa Udhibiti Ubora  na Majaribio  (TFRA) amekuwa akipokea wageni mbalimbali  katika vipando hivyo na kutoa maelezo  ya kitaalam kwa wakulima


  Wakulima wakifumdishwa matumizi sahihi ya Mbolea kwa vitendo


Wakulima mbalimbali wakiwa wanapata elimu ya matumizi ya mbolea kwenye vipando vya TFRA
Wanafunzi wa shule ya Sekondari Dodoma wakipata elimu ya matumizi sahihi ya mbolea kwenye zao la Alizeti

Post a Comment

Previous Post Next Post