BRELA YASHIRIKI MAONESHO YA UTAFITI NA UBUNIFU



 Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) inashiriki katika maonesho ya wiki ya Utafiti na Ubunifu yaliyoandaliwa na Chuo kikuu cha Dar es salaam.

Maonesho hayo ya siku tatu yanayofanyika katika  Shule ya Uhandisi na Teknolojia ya Chuo Kikuu cha Dar e Salaam, yanahusisha tafiti na bunifu mbalimbali ambazo zimefanywa na wavumbuzi.

Akitoa mchango wake katika Semina  ya Wahadhiri na Wanafunzi wa Fani za Teknolojia, Afisa Mwandamizi kutoka BRELA  Bw. Raphael Mtalima amewashuri   kuhakikisha kuwa bunifu mbalimbali zinazofanyika haziishii katika nadharia bali zisajiliwe na kuingizwa katika mchakato rasmi ili Utafiti na Ubunifu uzidi kukua kwa Ustawi wa uchumi wa Tanzania.

Bw. Mtalima amewahimiza pia watafiti wanaotarajia kuingiza bidhaa au bunifu zao sokoni   kuzisajili BRELA kupitia  huduma ya usajili  kwa njia ya mtandao.

BRELA itaendelea kutoa mafunzo na kuwafikia wabunifu mbalimbali katika maonesho hayo yatakayo hitimishwa April 14, 2023.

Post a Comment

Previous Post Next Post