WANACHUO MZUMBE WAPATIWA ELIMU YA MILIKI UBUNIFU





Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni BRELA inaendesha mafunzo katika vyuo mbalimbali jijini Mbeya ili kuongeza uelewa kuhusu Miliki Ubunifu.

Akizungumza katika Mafunzo hayo leo tarehe 18 Aprili, 2023 katika Chuo  Kikuu cha  Mzumbe Jijini Mbeya, Afisa Sheria kutoka BRELA Bw. Abdulkarim Nzori amesema Bunifu mbalimbali zikitumiwa zinaweza kutatua changamoto katika jamii na kuwakuza kiuchumi wabunifu na wafanyabiashara.

Katika mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na  wanafunzi zaidi ya  1000, wameelekezwa namna wanavyo weza tumia bunifu zao kujikwamua kiuchumi na kutengeneza ajira kwa watu wengine. 

Wanafunzi hao pia wamepata  fursa ya kukumbushwa kuwa Miliki Ubunifu ni mali inayotokana na mtu kutumia akili kubuni vitu mbalimbali hivyo wabunifu na wafanyabiashara wanayo nafasi kutumia bunifu zao kama vile Alama za Biashara na Huduma zilizosajiliwa BRELA  kutambulisha bidhaa au huduma wanazitoa na wanaweza kuziuza au kuzikodisha  Alama hizo pale inapobidi hivyo kunufaika na bunifu zao.

Awali akitoa neno la utangulizi Afisa Sheria kutoka BRELA Bi. Grace Umoti amewahamasisha wanafunzi hao kuchangamkia fursa ya ufadhili wa masomo ya Shahada ya Uzamili katika fani ya Miliki Ubunifu inayotolewa na BRELA pindi nafasi hizo  zinapotangazwa  ili kujiongezea ujuzi na kupanua wigo wa watalamu katika nyanja ya Miliki Ubunifu

Maafisa wa BRELA  wanaendelea kutoa Mafunzo katika Vyuo Vikuu na vyuo vya Mafunzo ya ufundi stadi (VETA)  na Shirika la Kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) katika Jiji la Mbeya

Post a Comment

Previous Post Next Post